wiz kid ft Drake ojuelegba (remex)
Tuesday, 21 July 2015
UANDIKISHAJI WA KUPIGA KURA KWA UCHAGUZI WA URAIS KWA MASHINE ZA BVR
Baadhi ya mashine za uandikishaji wa kupiga kura BVR
Mgombea wa urais wa Chadema akijiandikisha kupiga kura
Baadhi ya wananchi wakijiandikisha kupiga kura kwa kutumia mashine za BVR
Friday, 17 July 2015
BREAKING NEWZ!!!!! MWANAMUZIKI WA DANCE BANZA STONE AFARIKI
Muimbaji wa muziki wa dansi aliyewahi kutamba akiwa na bendi mbalimbali zikiwemo Twanga Pepeta na TOT Band, Ramadhan Masanja maarufu kama Banza Stone amefariki dunia mchana wa Ijumaa, July 17.
Banza alikuwa amelazwa kwenye hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam. Taarifa kuhusu kifo chake zimethibitishwa na kaka yake pamoja na mmiliki wa Twanga Pepeta, Asha Baraka.
Kwa mujibu wa kaka yake, Jabir Masanja, msanii huyo alikuwa anasumbuliwa na fangasi kichwani mwake na dawa alizokuwa anatumia zilikuwa kali kiasi cha kumpotezea hamu ya kula.
Hivi karibuni mama yake mzazi aliongea na kituo cha redio cha EFM na kukiambia kuwa afya ya mwanae ilizidi kuzorota na alianza kugoma kula chakula wala kunywa kunywa dawa. Mama huyo alisema hadi siku hiyo Banza alikuwa amegoma kula kwa siku tatu mfululizo.
Aliongeza kuwa pamoja na kuugua hivyo bado wasanii wenzake walishindwa kwenda kumjulia hali.
“Mpaka sasa sijamuona mtu yeyote aliyekuja kumshughulikia na kumwangalia, wamemwacha hivi hivi. Na mimi siwezi kuwalaumu kwanini hamjaja kumwangalia, kila mtu na moyo wake, mwenye kuja atakuja, mimi ntahangaika na mtoto wangu mpaka pale atakapoamua mwenyezi Mungu,” alisema Mama Banza.
Kabla ya hapo muimbaji huyo alizushiwa kufariki mara nyingi. Wiki chache zilizopita Banza alimongea na kipindi cha Leo Tena cha Clouds FM kukanusha.
“Ndio naumwa kichwa kina nisumbua sana lakini sasa hivi naendelea vizuri yaani hizo habari za kuzushiwa kifo naona sasa hivi kwangu sijui hata itakuwa mara ya ngapi, maana nimeshazushiwa sana. Mimi mzima na huyo anayeeneza azunguke na mikoa mingine aeneze vizuri,” alisema Banza.
“Lakini mimi nipo nyumbani hapa Sinza kwa Mama yangu sasa hivi hapa napata juice yaani marehumu anaongea,” aliongeza Banza kwa kicheko.
“Inshallah nikiwa vizuri mashabiki wangu wataniona tu lakini nipo mzima.”
Msiba upo nyumbani kwao Sinza, Dar es Salaam. Kwa wale wanaopenda kuchangia msiba wake wanaweza kumchangia kwa kutumia namba: 0715407088 au 0753786016.
Mungu ailaze mahali pema peponi. Amen.
Makuka jr(Admin)
Wednesday, 15 July 2015
MAPOKEZI YA DK. MAGUFULI YATIGISHA DAR, WANANCHI KWA MAELFU WAFURIKA VIWANJA VYA ZAKHEM, MBAGALA KUMSHUHUDIA
Mgombea wa nafasi ya Urais kupitia CCM Dk.John Pombe Magufuli akisalimiana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakati wa mapokezi kwenye uwanja wa ndege wa Dar es salaam.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar Es Salaam akimpokea Mgombea wa nafasi ya Urais kupitia CCM Dk.John Pombe Magufuli mara baada ya kuwasili jijini Dar es Salaam tayari kwa kujitambulisha kwa wakazi wa jiji hilo.
Dk. Magufuli akizungumza wakati wa mapokezi yake, kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwahutubia maelfu ya wananchi waliofika kumshuhudia Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Magufuli kwenye Viwanja vya Zakhem, Mbagala Dar es Salaam,
Wakazi wa Mbagala wakiwa wamejipanga barabarani kumuona mgombea wa Urais kupitia CCM Dk.John Pombe Magufuli
Katibu wa Itikadi na uenezi Nape Nnauye akiwasili kwenye viwanja vya Zakheem Mbagala akiwa kwenye usafiri wa Boda boda.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwasalimu wakazi wa jiji la Dar es Salaam waliojitokeza kwa wingi kumsikiliza mgombea wa nafasi ya Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli.
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk.John Pombe Magufuli akiwasili kwenye uwanja wa mkutano wa Mbagala Zakheem tayari kwa kujitambulisha kwa wakazi wa Dar es Salaam.
Dk. John Pombe Magufuli mgombea wa Urais kupitia CCM akisalimiana na Mbunge wa Jimbo la Kinondoni Mheshimiwa Idd Azzan wakati akiwasili kwenye uwanja wa mikutano Zakheem Mbagala.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam Ndugu Ramadhan Madabida akiwasalimu wakazi wa jiji la Dar es Salaam waliojitokeza kwenye mkutano wa kumtambulisha mgombea wa Urais wa CCM Dk. John Pombe Magufuli kwa wakazi wa Dar es Salaam.
Mgobea Urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Magufuli na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye wakizicharaza tumba, kusaidia wakati bendi ya TOT Plus ilipokuwa ikitumbuiza wakati wa mapokezi ya mgombea huyo kwenye Viwanja vya Zakhem Mbagala Dar es Salaam leo
Picha na (Makuka jr)
Tuesday, 14 July 2015
UVAMIZI WA KITUO CHA POLISI CHA STAKISHARI
Ni taarifa ambazo zimechukua headlines usiku wa July 12 baada ya watu wanaosadikiwa kuvamia kituo cha polisi cha Stakishari kilichopo Ukonga Dar na kuuwa watu saba.
Kwa mujibu wa Mkuu wa polisi (IGP), Ernest Mangu…’Nasikitika kuwapa taarifa kuwa majambazi walivamia kituo cha polisi cha stakishari na kupiga risasi na kuua Askari polisi wanne na raia watatu. Majambazi hao walikuja kama raia wakawaida wanaohitaji huduma walipofika kituoni na kuulizwa shida yao nini ndipo walipoanza kuwashambulia askari walio kuwa kituoni
Raia waliouwawa ni raia ambao walikuwa wamekuja kituoni kutoa taarifa za matukio ya kwao ya kawaida wapo pia askari ambao wamejeruhiwa na raia waliojeruhiwa wapo hospitali wanapata matibabu
Nikweli kuna silaha ambazo zimeporwa miongoni ni zile ambazo za askari ambao walikuwa ulinzi hapa na zingine zilikuwa chumba cha mashitaka.uchunguzi unaendelea kujua silaha ngapi zimeporwa wakati tukipata taarifa mpya tutazitoa
Tukio hilo la kusikitisha lazima sheria ichukue mkondo wake kuwapata hao waliohusika na tukio hilo.kama mnakumbuka tukio kama hili lilitokea Ushirombo walivamia kituo kama hiki walisababisha mauaji kwa Askari sisi hatutachoka tutahakikisha tunapambana nao mpaka tunawapata
Nibaadhi ya silaha ambozo zilihusika katika mapambano kati ya polisi na majambazi katika kituo cha polisi
Picha na Abduly Makuka jr
Subscribe to:
Posts (Atom)