Angalia mwendelezo wa series ya the empire online kwenye link hiyo
Monday, 28 December 2015
Tuesday, 21 July 2015
UANDIKISHAJI WA KUPIGA KURA KWA UCHAGUZI WA URAIS KWA MASHINE ZA BVR
Baadhi ya mashine za uandikishaji wa kupiga kura BVR
Mgombea wa urais wa Chadema akijiandikisha kupiga kura
Baadhi ya wananchi wakijiandikisha kupiga kura kwa kutumia mashine za BVR
Friday, 17 July 2015
BREAKING NEWZ!!!!! MWANAMUZIKI WA DANCE BANZA STONE AFARIKI
Muimbaji wa muziki wa dansi aliyewahi kutamba akiwa na bendi mbalimbali zikiwemo Twanga Pepeta na TOT Band, Ramadhan Masanja maarufu kama Banza Stone amefariki dunia mchana wa Ijumaa, July 17.
Banza alikuwa amelazwa kwenye hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam. Taarifa kuhusu kifo chake zimethibitishwa na kaka yake pamoja na mmiliki wa Twanga Pepeta, Asha Baraka.
Kwa mujibu wa kaka yake, Jabir Masanja, msanii huyo alikuwa anasumbuliwa na fangasi kichwani mwake na dawa alizokuwa anatumia zilikuwa kali kiasi cha kumpotezea hamu ya kula.
Hivi karibuni mama yake mzazi aliongea na kituo cha redio cha EFM na kukiambia kuwa afya ya mwanae ilizidi kuzorota na alianza kugoma kula chakula wala kunywa kunywa dawa. Mama huyo alisema hadi siku hiyo Banza alikuwa amegoma kula kwa siku tatu mfululizo.
Aliongeza kuwa pamoja na kuugua hivyo bado wasanii wenzake walishindwa kwenda kumjulia hali.
“Mpaka sasa sijamuona mtu yeyote aliyekuja kumshughulikia na kumwangalia, wamemwacha hivi hivi. Na mimi siwezi kuwalaumu kwanini hamjaja kumwangalia, kila mtu na moyo wake, mwenye kuja atakuja, mimi ntahangaika na mtoto wangu mpaka pale atakapoamua mwenyezi Mungu,” alisema Mama Banza.
Kabla ya hapo muimbaji huyo alizushiwa kufariki mara nyingi. Wiki chache zilizopita Banza alimongea na kipindi cha Leo Tena cha Clouds FM kukanusha.
“Ndio naumwa kichwa kina nisumbua sana lakini sasa hivi naendelea vizuri yaani hizo habari za kuzushiwa kifo naona sasa hivi kwangu sijui hata itakuwa mara ya ngapi, maana nimeshazushiwa sana. Mimi mzima na huyo anayeeneza azunguke na mikoa mingine aeneze vizuri,” alisema Banza.
“Lakini mimi nipo nyumbani hapa Sinza kwa Mama yangu sasa hivi hapa napata juice yaani marehumu anaongea,” aliongeza Banza kwa kicheko.
“Inshallah nikiwa vizuri mashabiki wangu wataniona tu lakini nipo mzima.”
Msiba upo nyumbani kwao Sinza, Dar es Salaam. Kwa wale wanaopenda kuchangia msiba wake wanaweza kumchangia kwa kutumia namba: 0715407088 au 0753786016.
Mungu ailaze mahali pema peponi. Amen.
Makuka jr(Admin)
Wednesday, 15 July 2015
MAPOKEZI YA DK. MAGUFULI YATIGISHA DAR, WANANCHI KWA MAELFU WAFURIKA VIWANJA VYA ZAKHEM, MBAGALA KUMSHUHUDIA
Mgombea wa nafasi ya Urais kupitia CCM Dk.John Pombe Magufuli akisalimiana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakati wa mapokezi kwenye uwanja wa ndege wa Dar es salaam.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar Es Salaam akimpokea Mgombea wa nafasi ya Urais kupitia CCM Dk.John Pombe Magufuli mara baada ya kuwasili jijini Dar es Salaam tayari kwa kujitambulisha kwa wakazi wa jiji hilo.
Dk. Magufuli akizungumza wakati wa mapokezi yake, kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwahutubia maelfu ya wananchi waliofika kumshuhudia Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Magufuli kwenye Viwanja vya Zakhem, Mbagala Dar es Salaam,
Wakazi wa Mbagala wakiwa wamejipanga barabarani kumuona mgombea wa Urais kupitia CCM Dk.John Pombe Magufuli
Katibu wa Itikadi na uenezi Nape Nnauye akiwasili kwenye viwanja vya Zakheem Mbagala akiwa kwenye usafiri wa Boda boda.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwasalimu wakazi wa jiji la Dar es Salaam waliojitokeza kwa wingi kumsikiliza mgombea wa nafasi ya Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli.
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk.John Pombe Magufuli akiwasili kwenye uwanja wa mkutano wa Mbagala Zakheem tayari kwa kujitambulisha kwa wakazi wa Dar es Salaam.
Dk. John Pombe Magufuli mgombea wa Urais kupitia CCM akisalimiana na Mbunge wa Jimbo la Kinondoni Mheshimiwa Idd Azzan wakati akiwasili kwenye uwanja wa mikutano Zakheem Mbagala.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam Ndugu Ramadhan Madabida akiwasalimu wakazi wa jiji la Dar es Salaam waliojitokeza kwenye mkutano wa kumtambulisha mgombea wa Urais wa CCM Dk. John Pombe Magufuli kwa wakazi wa Dar es Salaam.
Mgobea Urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Magufuli na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye wakizicharaza tumba, kusaidia wakati bendi ya TOT Plus ilipokuwa ikitumbuiza wakati wa mapokezi ya mgombea huyo kwenye Viwanja vya Zakhem Mbagala Dar es Salaam leo
Picha na (Makuka jr)
Tuesday, 14 July 2015
UVAMIZI WA KITUO CHA POLISI CHA STAKISHARI
Ni taarifa ambazo zimechukua headlines usiku wa July 12 baada ya watu wanaosadikiwa kuvamia kituo cha polisi cha Stakishari kilichopo Ukonga Dar na kuuwa watu saba.
Kwa mujibu wa Mkuu wa polisi (IGP), Ernest Mangu…’Nasikitika kuwapa taarifa kuwa majambazi walivamia kituo cha polisi cha stakishari na kupiga risasi na kuua Askari polisi wanne na raia watatu. Majambazi hao walikuja kama raia wakawaida wanaohitaji huduma walipofika kituoni na kuulizwa shida yao nini ndipo walipoanza kuwashambulia askari walio kuwa kituoni
Raia waliouwawa ni raia ambao walikuwa wamekuja kituoni kutoa taarifa za matukio ya kwao ya kawaida wapo pia askari ambao wamejeruhiwa na raia waliojeruhiwa wapo hospitali wanapata matibabu
Nikweli kuna silaha ambazo zimeporwa miongoni ni zile ambazo za askari ambao walikuwa ulinzi hapa na zingine zilikuwa chumba cha mashitaka.uchunguzi unaendelea kujua silaha ngapi zimeporwa wakati tukipata taarifa mpya tutazitoa
Tukio hilo la kusikitisha lazima sheria ichukue mkondo wake kuwapata hao waliohusika na tukio hilo.kama mnakumbuka tukio kama hili lilitokea Ushirombo walivamia kituo kama hiki walisababisha mauaji kwa Askari sisi hatutachoka tutahakikisha tunapambana nao mpaka tunawapata
Nibaadhi ya silaha ambozo zilihusika katika mapambano kati ya polisi na majambazi katika kituo cha polisi
Picha na Abduly Makuka jr
Tuesday, 5 May 2015
Mayweather amchapa Paquiao
Hatimaye bondia FLOYDE MAYWEATHER aibuka kidedea kwa kushinda pambano dhidi ya PAQUIAO na kutwaa ubingwa wa WFB,HBO,PBO kwa points
Ushahidi wa Majaji wa Mpambano huo wakionesha matokeo ya mchezo huo ingawa watu wanasema kuwa FLOYDE MAYWEATHER hakushinda kihalali.
(picha na Makuka jr)
Rekodi za mabondia kati ya Paquiao na Mayweather
Ni baadhi ya rekodi za mabondia hao. je? Nani ataibuka kidedea na kuweka historia ya Dunia usikose kufatilia blog yetu ya harakati za Mtaa kwa taarifa muhimu zaidi
Mpambano mkali wa Dunia
Ule mpambano wa masubwi wa Dunia kati ya Bondia wa Philpino Manny Pacquiao na Marekani Floyde Mayweather umekaribi ambapo leo mabondiaa hao wamepima uzito na kutambiana
Saturday, 28 March 2015
MWANZILISHI WA TIP TOP CONNECTION ABDU BONGE AFARIKI DUNIA
Aliyekuwa meneja na Mwanzilishi wa Tip top connection ABDU BONGE amefariki
dunia jana mach 28.
Kwa Mujibu wa chanzo chetu cha habari Abdu Bonge alikuwa akiugua
Harakati za mtaa blog Chini ya DOP Dully zinatoa pole kwa familia ya Bonge na Wafiwa
wote mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi Amin
Bwana ametoa na Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe
Tutawaletea Habari Zaidi
dunia jana mach 28.
Kwa Mujibu wa chanzo chetu cha habari Abdu Bonge alikuwa akiugua
Harakati za mtaa blog Chini ya DOP Dully zinatoa pole kwa familia ya Bonge na Wafiwa
wote mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi Amin
Bwana ametoa na Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe
Tutawaletea Habari Zaidi
RAIS WA ZIMBABWE ROBERT MUGABE AFUNGUA KONGAMANO LA VIJANA AFRIKA NA CHINA,RAIS KIKWETE ATUNUKIWA TUZO YA HESHIMA
Mgeni rasmi wa Kongamano la tatu la Viongozi vijana wa Afrika na China,Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe akihutubia usiku wa jana kwenye kongamano hilo lililo fanyika katika Ukumbi wa Mikutano Ngurdoto Arusha
Katibu mkuu wa CCM, Ndugu Abraham Kinana akizungumza katika kongamano hilo mbele ya mgeni rasmi Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe
Rais kikwete akitoa salamu zake kwa washiriki wa kongamano la tatu la Viongozi Vijana wa Afrika na China,Ambalo mgeni rasmi alikuwa ni Rais wa Zimbabwe
Rais Jakaya kikwete akipewa tuzo ya heshima juu ya kuhamasisha Amni na utulivu Barani Afrika na Rais wa Umoja wa Vijana Afrika
(PAYU) Francine Furaha Muyumba.Tuzo hiyo imetolewa na umoja wa Vijana wa Afrika,pichani kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Mufindi
Mh. Mboni Mhita
Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Baadhi ya washiriki wa Kongamano la tatu la umoja wa viongozi vijana wa Afrika na China,Ambapo Mgeni rasmi alikua ni Rais wa Zimbabwe
Mh. Robert Mugabe
Rais Kikwete akizungumza jambo na katibu mkuu wa CCM ndug Kinana alipo wasili jioni ya jana
katika moja ya ukumbi wa mikutano hoteli ya Ngurdoto mjini Arusha, kwa ajili ya kutoa salamu kwa washiriki wa kongamano la Viongozi Vijana wa Afrika na China
Ambalo mgeni Rasmi alikua ni Raiswa Zimbabwe ,Robert Mugabe
Pichani kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya makamu wa Rais -Mazingira Mh. Stephan Masele.
Picha zote na (DOP Abduly Makuka)
Friday, 27 March 2015
Pasaka! Pasaka ! Pasaka!
IT'S ALL ABOUT MUSIC
Chiwileinc Entertainment inakudondoshea show la kibaba likihusisha Amir mill, Fraga de Pro Sam Flavour Mwailonda Masia, Y-sam, Claver B, Masai wa kigoma Nzasa Hood & Dienova, siku ya Pasaka katika ukumbi wa Manchester Pub mbagala dar es salaam kwa kiingilio cha #3000 wanaume wakati wadada watachangia #2000 tu hii ndio nafasi kuja kucheza nikupeti peti na Dunia mzima Live Bila kusahau mixng kali toka kwa ma Dj DOP Kukaa
Chiwileinc Entertainment inakudondoshea show la kibaba likihusisha Amir mill, Fraga de Pro Sam Flavour Mwailonda Masia, Y-sam, Claver B, Masai wa kigoma Nzasa Hood & Dienova, siku ya Pasaka katika ukumbi wa Manchester Pub mbagala dar es salaam kwa kiingilio cha #3000 wanaume wakati wadada watachangia #2000 tu hii ndio nafasi kuja kucheza nikupeti peti na Dunia mzima Live Bila kusahau mixng kali toka kwa ma Dj DOP Kukaa
MSAKO MKALI
Waganga wa Jadi Wawapinga Mkwara Jeshi la Polisi, Wasema Tabia ya Kufanya Msako na Kuchukua Vibuyu vya Itawatokea Puani
Wakati msako wa kuwakamata waganga wapiga ramli chonganishi ukiendelea nchi nzima CHEKI HAPA=>http://bit.ly/1zZzENW hasa katika mikoa ya kanda ziwa, jeshi la polisi nchini limepewa onyo toka kwa wanganga wa jadi juu ya vifaa vinavyokamatwa wakati wa msako wao.CHEKI HAPA=>http://bitly.com/1MBFSf4
Wakati msako wa kuwakamata waganga wapiga ramli chonganishi ukiendelea nchi nzima CHEKI HAPA=>http://bit.ly/1zZzENW hasa katika mikoa ya kanda ziwa, jeshi la polisi nchini limepewa onyo toka kwa wanganga wa jadi juu ya vifaa vinavyokamatwa wakati wa msako wao.CHEKI HAPA=>http://bitly.com/1MBFSf4
Thursday, 26 March 2015
Subscribe to:
Posts (Atom)